Monday, October 3, 2016

Tambua jinsi ya kujikwamua kiuchumi wewe mwanakagera kupitia kwa wadau wa elimu.

Na Lameck Richard-BUKOBA

Tambua jinsi ya kujikwamua kiuchumi wewe  mwanakagera kupitia kwa wadau wa elimu.
  Kutokana na wimbi kubwa la vijana kukumbana na changamoto ya kukosa ajira pindi wanapohitimu masomo yao katika vyuo mbalimbali mkoani Kagera na Tanzania kwa ujumla, hali inayopelekea kuwepo kwa makundi ambayo yanaweza kuhatarisha maisha ya wnanchi kwa sababu ya kukosa kazi ya kufanya.
   Gazeti hili liliongea na mdau wa elimu mkoani kagera pia mkurugenzi wa chuo cha King Rumanyika Bw.Godison Rwegasira, ambapo alisema kuwa kuna changamoto kubwa inayowakabili wahitimu wa vyuo mbalimbali huku akisema kuwa wahitimu hao wanajisahau kujihusisha hata na kazi za ujasiliamali,na pengine kwa kutopata elimu hiyo kutoka waliposomea au kutofatilia.
    Bw.Godison alisema kuwawao wameanzisha taasisi ya elimu kwa lengo la kuondoa ujinga katika taifa letu na kuwasaidia vijana kuajiriwa au kujiajiri na kuwasaidie wananchi wengine ikiwa ni pamoja  na kujikwamua kiuchumi kupitia ajira wanazozipata.
  Kupitia hilo aliwashauri wadau wengine wa elimu na wamiliki wa vyuo mkoani kagera kuhakikisha wanatoa hata elimu ya ujasiliamali kwa wanafunzi wao  kwa ajili ya kuwawekea mazingira mazuri wahitimu ili pindi wanapokuwa nyumbani wakisubiria
 kuajiriwa wawe wanaendelea na majukumu mengine.
Aliwashauri  vijana wote waliobahatika  kwenda vyuoni kuacha tabia ya kulalamika sana kuwa hawana la kufanya kutoka na ajira kuchelewa,kwani watambue kuwa kuna mambo mengi ya kufanya katika jamii kwa kutumia elimu walioipata na aliongeza kuwa hata wale ambao pengine kwa bahati mbaya hawakuweza kujiendeleza miradi. Alisema kuwa hata kilimo,taasisi binafsi kielimu wasikae ndani kwa kudai kuwa hamna kazi kwani watambue kunani sehemu moja wapo iliyowasaidia watu wengi kutoka kimaisha,hivyo vijana wasidharau kazi  na wasipendelee kuwa na mafanikio ya muda huo huo,bali wawekeze kwanza ili baadae waweze kunufaika na kile watakachokianzisha na pale watakaposhindwa wanaweza kuongea na hao wadau wa maendeleo au watu waliopiga hatua kimaisha ili kuhakikisha wanasonga mbele kimaendeleo.

   Bw.Godison aliongeza kuwa pamoja na hayo  waajiriwa wote na wanaojiajiri wanatakiwa kuhakikisha wanatanguliza  nidhamu kazini pindi wanapokuwa wanatekeleza majukumu yao ya kazi,sanasana alisema kuwa wale wanaoajiriwa wanatakiwa kuwa makini sana kwenye majukumu yao kwani tofauti na hapo wanaweza  kujikuta  wanaachishwa kazi hususani kipindi hiki cha “hapa kazi tu”.
Pichani: Bwana Godison Rwegasira, Mkurugenzi wa chuo cha King Rumanyika kilichopo Manispaa  ya Bukoba Mkoani Kagera



No comments:

Post a Comment