Monday, October 3, 2016

Kufungwa kwa KAT Wazee wa Torrent Kuisoma Namba

NA DIDAS MUGYABUSO

Kwa wenzangu wataalamu wa masuala ya ICT hili habari sio ngeni kwao, ule uwanja wetu pendwa wa kupakua kilakitu bure ‘KickAss Torrent (KAT)’  haupo tena nasi, tovuti hii iliyojizolea umaarufu kwa takribani miaka 8, ilituwezesha kushusha ‘ku-download’ Programu mbalimbali, Muvi, Vitabu,Games, Miziki, n.k, hii ilitokea mnamo tarehe 20 Julai mwakahuu, na ilikuwa ni pigo kubwa sana kwa walevi wa mtandao huu. Ni pigo kwakuwa ni watu wengi sana walikuwa wakiutegemea huu uwanja kuendesha shughuli zao, kwa mfano kwa hapa Tanzania ni watumiaji wachache wa kompyuta ambao wamekuwa na spirit ya kutoa dola 20 hadi 100 kwa ajili ya kununua Antivirus, ama dola 100 hadi 300 kwa ajili ya kununua Window na programu nyingine za Kompyuta. Hata ukienda kwa mafundi wa Kompyuta programu nyingi wanazotumia kwa wateja sio ‘Genuine’, nyingi ndo hizi tunazozitoa kwenye tovuti za wizi kama hii KAT, kwa  ‘maana hiyo ni wengi tutaisoma namba’ kwenye hili.
Nani kaufunga? Mtandao huu umefungwa na Marekani kwa kosa la kusambaza ‘contents’zenye thamani ya zaidi ya $1 bilioni kinyume na sheria.Lakini huu sio mtandao wa kwanza kufungwa na Marekani, mitandao kadhaa kama The Piratebay uliwahi kufungwa miaka michache iliyopita
Nani Mmiliki wa KAT? Ni Artem Vaulin kijana wa miaka 30, raia wa Ukraine, alikamatwa akiwa nchini Poland. Kijana huyu alitengeneza dola milioni 12 kwa mwaka kutokana Na matangazo kupitia KAT.
kampuni ya Facebook na Apple Inc washiriki katika kukamatwa kwa Vaulin Mchakato ulianzia kwa IRS agent kuomba kuweka matangazo kwenye tovuti ya KAT, makubaliano yaliyofanyika baina ya mmiliki wa KAT na mwakilishi rasmi wa kampuni ya IRS agent. Tangazo lilipoanza kwenda hewani, iliwapa nafasi IRS ku’track’taarifa za kutosha kuweza kuhusisha KAT  na akaunti ya benki ya Latvian. akaunti ambayo baadaye iligundulika wamepokea takriban dola milioni 31 katika amana kati ya Agosti mwaka 2015 na Machi 2016.

Baada ya uchunguzi mkali wa hapa na pale, timu hiyo ya wakaguzi iliweza kutambua email ambayo alikuwa si tu na uhusiano na tovuti, lakini pia katika channel rasmi za tovuti katika mitandao ya kijamii ikiwa ni pamoja na Facebook.

Hatua iliyofuata Apple walijaribu kukamilisha mchezo kwa kutoa taarifa ambayo inawezekana ndiyo ilikaba shughuli zote za akaunti ya Apple iliyokuwa ikimilikiwa na Vaulin.

“Records provided by Apple showed that tirm@me.com conducted an iTunes transaction using IP Address 109.86.226.203 on or about July 31, 2015. The same IP Address was used on the same day to login into the KAT Facebook Account. Then, on or about December 9, 2015, tirm@me.com used IP Address 78.108.181.81 to conduct another iTunes transaction. The same IP Address was logged as accessing the KAT Facebook Account on or about December 4, 2015.”
Apple walitoa taarifa Julai31, 2015 kuonyesha kwamba ku email hiyo ilitumika nunulia kitu kwenye iTunes na kisha IP address hiyohiyo ikatumiwa kupata access kwenye ukurasa wa Facebook wa KAT.
Kwa ufupi hivyo ndivyo muvi ya KAT ilipoishia. Je, kutapatikana mbadala wake ama ndio tutaendelea kuisoma namba?



No comments:

Post a Comment