Tuesday, September 20, 2016

"Nina nyimbo zaidi ya 90"- Nshomile

Israel Didas(Nshomile Family), msanii wa nyimbo za asili Bukoba




NA HAMASA
Nshomile Family sio jina geni kwa wakazi wa  Mkoa wa Kagera, ni kundi lililopata kutamba Mkoani humo kutokana na kazi mbalimbali walizozifanya. Kundi hilo linaundwa na wasanii wawili Israel Didas na Ras Voice. Gazeti hili la HAMASA Lilipiga  stori na Israel Didas ambaye ni memba wa kundi hilo, alisema mziki alianza rasmi mwaka 2008, ana album moja sasa,  msanii huyo wa miondoko ya Afropop Alisema mziki alianza kufanya akiwa shule ya msingi baada ya kugundua kipaji chake, kabla ya kuingia studio alikuwa akifanya show mbalimbali za jukwaani zikiwemo show za kampeni ambapo zilimuwezesha kujilipia mwenyewe studio. Wimbo uliomtambulisha katika game ni Ondeke (Uniache) alioufanyia studio ya Mwanza inayoitwa Kivuli
“Mwanzo nilianza kwa kuimba nyimbo za kawaida kwa Lugha ya Kiswahili, baadaye nikaamua niwe natumia kihaya kwenye nyimbo zangu baada ya kugundua nakubalika zaidi upande huo wa nyimbo za asili” Aliendelea. Akijibu swali la mwandishi anasema si lazima msanii wa Kagera aimbe kihaya ndio atoke, kwani wasanii kama BK Sunday na Shemela walitambulika kwa kuimba nyimbo za Kiswahili kabla hawajabadilika na kujikita kwenye kihaya.
Aliendelea kusema kuwa kwa sasa amekuwa hasikiki sana kutokana na matatizo ya kifamilia, hata hivyo ana nyimbo mpya ambazo zinaendelea  kuchezwa na vituo mbalimbali vya redio na tv, nyimbo hizo ni Ndo Hao na Kajakaro. Anaamini  kwa Tanzania msanii hawezi kufanikiwa kwa kiasi kikubwa bila kwenda Dar ambapo kuna  media na studio kubwa, hivyo akipata mtu wa kumuwezesha na kusimamia kazi zake atafanya hivyo kwani ana nyimbo nyingi sana.
“Nina nyimbo zaidi ya 90 ambazo bado hazijarekodiwa”, aliongeza.

Mafanikio aliyopata kwenye mziki ni kujulikana na pia unamuwezesha kujikimu kimaisha, kwani hupata mialiko sehemu mbalimbali kama kwenye, maharusi, mijuburo, matamasha mbalimbali , n.k. 
Kuhusu sanaa ya  Mkoa wa Kagera kwa sasa anasema haina mwelekeo, ni kama wasanii wametelekezwa, kwani hakuna watu wa kusimamia kazi zao kama ilivyokuwa huko nyuma enzi za kina Saida Karoli ambao walitamba na nyimbo mbalimbali kama chambua kama karanga. Msanii wa Mkoa wa Kagera anae mkubali kwa sasa ni Sarah wa Kakau Band, na msanii chipukizi anayemkubali ni Molly P ambapo alisema kuwa  anamshukuru Mungu kwani mashabiki wamekuwa wakizipokea vizuri sana kazi zake, kitu kinachomkwamisha ni wadau wa kumuwezesha ili aweze kusonga mbele zaidi. Alisema kuwa  anaupenda sana mziki na anahisi bado anaudai, na anawapenda sana mashabiki zake, vilevile amewaomba waendelee kuwasapoti wasanii wa nyumbani wanaofanya vizuri.

2 comments:

  1. Johanesboy msanii mkubwa kagera nyimbo mpya JOHANESBOY mungu anakuona

    ReplyDelete
  2. Johanesboy nyimbo mpya johanesboy mungu anakuona hatuioni kagera

    ReplyDelete