Tuesday, September 20, 2016

Maua arudi kivingine




NA HAMASA

Mmoja kati ya wanamuziki wakongwe na mahiri mkoani Kagera Maua Chenkula akizungumza na HAMASA alizungumzia ujio wake mpya katika gemu la muziki wa asili vilevile soko la muziki wa asili Mkoa wa Kagera na Tanzania kwa  ujumla, hiki ndicho alicho kisema “Nawaomba  mashabiki  zangu waelewe kwamba sijaacha  Muziki ila nilisimama kutokana na matatizo,hata hivyo mwaka juzi nimetoa Albamu iitwayo TINKILYA ina nyimbo saba(7) zikiwa ni audio,vilevile mwaka jana nikazitolea video nyimbo zote saba (7) na kwa sasa nimetoa wimbo mpya unaitwa ENGONZI MILEMBE na tayari nimeutengenezea video ambayo itatoka muda wowote.Albamu yangu ya TINKILYA  inanyimbo saba ambazo ni Tinkilya, Kazoni, Tanzania, Ninsiima, Bandeke, Bakundekele na Nsheshe.” Msanii mkongwe wa nyimbo za asili aliongezea kwa kuainisha malengo yake katika Albamu yake ya TINKILYA, “Katika Albamu hii ya TINKILYAninamalengo ya kuendeleza muziki wa asili yetu ili usipotee na kuutangaza ndani na nje ya Tanzania ili waujue , kuitangaza Tanzania na mimi mwenyewe kujipatia kipato kupitia  albamu hiyo.”
Maua Chenkula ambaye aliuza sana kazi zake za nyimbo za asili kipindi cha miaka ya nyuma alizungumzia mabadiliko katika soko la muziki wa nyimbo za asili kwa kipindi hiki alisema,”Mabadiliko ni makubwa sana katika faida ya muziki wa asili mfano, zamani muziki wa asili ulikuwa hauna kipato ulikuwa unaburudisha na kuelimisha tu,laikini kwa sasa muziki wa asili unaelimisha pia unakupatia kipato.Muziki wa asili wa sasa umekuwa na thamani na jamii imeutambua kuwa ni kazi ,nami nawahakikishia kuwa muziki ni kazi kama kazi nyingine na unakipato kizuri.” Akiwa anamalizia mazungumzo yake na Gazeti  la Hamasa Mwanamuziki Maua Chenkula ambaye ni Mshindi wa Tuzo ya TMMT 2015-16 kama Muimbaji bora wa kike wa nyimbo za asili zilizotolewa Mjini Bukoba aliizungumzia tuzo hiyona kwa namna ilivyo muhamasisha katika kazi zake ,”Tuzo niliyopata niliifurahia sana na ilinihamasisha kuendeleza muziki wa asili maana niliona kuwa watu wananikubali Maua kama Maua  ndo maana walinichagua kuwa mshindi nawashukuru  sana mashabiki wangu na wapenzi wote wa nyimbo za asili kwa kunipa moyo  na ninawaahidi  wategemee mambo mazuri sana maana tayari nimejipanga  sawasawa na ninajua wimbo wangu mpya wa ENGONZI MILEMBE (Yaani upendo ni Aman) wataupenda una meseji nzuri sana na umetengenezwa ki utaalamu zaidi.”


No comments:

Post a Comment