Monday, October 3, 2016

HISTORIA YA MWANAMASUMBWI HAYATI MUHAMMAD ALI

NA DIDAS MUGYABUSO
(Kwa msaada wa Mtandao)


Hayati Muhammad Ali anayeaminika kuwa moja ya wanamasumbwi bora wa mda wote duniani alikuwa bondia kwa sababu kuna mtu aliyemuibia baskeli yake. Alikuwa na umri wa miaka 12 wakati ule na ali¬kuwa akiishi Louisville katika jimbo la Kentucky akijuilikana kwa jina la Cassius Mercellus Clay Jr.
Siku ya tukio hilo alikuwa na rafiki zake wakitafuta peremende na porp corns za bure.
Alipogundua kwamba baiskeli yake imeibiwa  aliagizwa kwende chini ya nyumba aliyokuwepo katika taasisi ya mafunzo ya Columbia ambapo afisa wa polisi Joe Martin alikuwa akisimamia mpango wa ndondi.Martin alimwelezea Ali kwamba aanze kunoa ngumi zake kwa kujifunza ndondi kabla ya kumtafuta mwizi huyo. Joe Martin, aliyekuja kuwa kocha wake baadaye, anaelezea jinsi kijana huyo alivyokuwa akilia huku akiahidi kumtandika ngumi aliyemuibia baiskeli yake pindi akimpata. Kocha huyo wa ubondia aliyekuwa Polisi wakati huo alimchukua Clay, kijana mweusi anayetokea katika familia ya watu maskini, na kumjumuisha na watoto wengine aliokuwa akiwafundisha.“Alikuwa na bidii zaidi kuliko waatoto wote wengine niliokuwa nikiwasimamia,” anasema Joe Martin.
Ingawa Clay wakati ule hakuwa na nguvu ya kuvurumisha masumbwi, alikuwa mwepesi wa kuranda randa kupita kiasi. Mnamo mwaka 1960, akiwa na umri wa miaka 18, alishinda katika pambano la ndondi la michezo ya Olympiki mjini Rome, Italia. Medali yake ya dhahabu inasemekana aliitupa ndani ya Mto Ohio kwa sababu alikasirishwa na jinsi watu weusi wanavyobaguliwa nchini mwake. Cassius Clay alikamilisha michuano ya wasiolipwa baada ya kuibuka na ushindi mara 100 katika jumla ya mapambano 108 aliyopigana. Wafanyabiashara 11 wa Kizungu kutoka Louisville walishirikiana ili kumfungulia njia Cassius Clay ya kuingia katika ulingo ya mabondia wa kulipwa.Bondia huyo mwenye kipaji alikuwa akijulikana pia kuwa ni mtu aliyekuwa na majivuno na mdomo mpana. Kabla ya mapambano yake, Cassius Clay daima alikuwa akijitapa kuwa yeye ndie mbabe wa wababe na mzuri

kuliko mabondia wote na kuwakejeli wapinzani wake. Mtindo ambao umekuwa ukitumiwa pia na mabondia wa kileo kama Floyd Mayweather, na hapa Tanzania umekuwa ukitumiwa na mabondia kama Mada Maugo na Francis Cheka. Katika pambano lake la kwanza la kuwania ubingwa wa dunia Februari 1964 dhidi ya mtetezi wa taji hilo, Sonny Liston, Clay hakuwa akijulikana ni nani na watu waliamini angeshindwa tu. Lakini baada ya raundi ya sita, Liston aliungama. “Mie ndie mbabe,” alinguruma Cassius Clay kupitia kipaza sauti.
Mwaka huo huo, alisilimu na kujiunga na kundi la Nation of Islam lililokuwa likiongozwa wakati huo na mwanaharakati wa haki wa Wamarekani Weusi, Malcolm X. Akabadilisha jina la Cassius Clay na kujiita wakati huo huo Muhammad Ali.Muhammad Ali hakuwa bondia tu, alikuwa mwanaharakati pia. Alipinga vita vya Marekani nchini Vietnam na alikataa kutekeleza sheria ya kutumikia jeshi. Mnamo mwaka 1967, akapokonywa sio tu leseni yake ya ubondia, bali pia alihukumiwa kifungo cha miaka mitano jela, ingawa baadaye bondia huyo wa aina pekee aliachiwa kwa dhamana.Wasanii na wasomi mfano wa Richard Burton na Henry Fonda au mwandishi vitabu Truman Capote wakampigania mpaka Muhammad Ali akaruhusiwa tena kurejea ulingoni baada ya kulazimika kukaa nje kwa miaka mitatu. Machi 8, 1971 Muhammad

Ali aliteremka ulingoni Madison Square Garden mjini New York kwa kile kilichotaajwa “kuwa pambano la ndondi la karne” dhidi ya bingwa wa wakati ule, Joe Frazier. Lilikuwa pambano kati ya mafahali wawili, kati ya mpinzani na yule aliyekuwa akiangaliwa kama mwakilishi wa mtindo wa maisha wa Kimarekani. Katika pambano hilo la kusisimua la zaidi ya raundi 15, Frazier akashinda kwa pointi. Ali akalazimika kwa mara ya kwanza katika maisha yake ya ubondia kunusa jamvi.
Yakafuata mapambano mengine ya kusisimua mfano wa lile la mjini Kinshasa dhidi ya George Foreman mnamo mwaka 1974, ambapo Muhammad Ali anasema aliranda mfano wa kipepeo na kuuma kama nyuki ‘Float like butterfly, sting like a bee’
Muhammad Ali alilipiza kisasi dhidi ya Joe Frazier mwaka 1975 na kumlazimisha kusalimu amri mnamo rauni ya 14. Mohammed Ali alistaafu mwishoni mwa mwaka 1981 baada ya kukaa ulingoni kwa zaidi ya miaka 25 .
Wakati huo tayari alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya Parkinson. Licha ya maradhi hayo, Muhammad Ali ndiye aliyewasha mwenge wa Olimpiki huko Atlanta mnamo mwaka 1996 na kuusisimua ulimwengu mzima. Mwaka 1999 aliteuliwa na kamati kuu ya michezo ya Olimpiki kuwa “mwanaspoti bora wa karne.”
Mpinzani wake wa zamani George Foreman amegeuka hivi sasa kuwa rafiki yake

mkubwa na kuungama “Muhammad Ali ndie bingwa wa mabingwa.” Mpaka June 4 2016 Muhhamad Ali anapoteza maisha ndie mwanamasumbwi mstaafu kutoka nchini Marekani. aliepata kuwa bingwa wa uzito wa juu mara tatu.

Je, mastaa wanasemaje kuhusu Muhammad Ali?
Haya ni maneno ya Rais wa zamani wa Marekani kipindi Ali anatimiza miaka 70 ya kuzaliwa;“Ustadi, haiba na misimamo isiyoyumba ya Muhammad Ali ndio mambo yaliyosaidia kuufanya mchezo wa masumbwi kuwa maarufu duniani”“Watu waliacha kuupenda mchezo wa ngumi. Katika miaka ya 1940 na 1950 ulikuwa ni mchezo maarufu sana Marekani na baadae umaarufu huo ukapotea,” aliimwambia mtangazaji wa masumbwi wa BBC Mike Costello.
“Baadae akachomoza Muhammad Ali, awali akiitwa Cassius Clay, akionekana sawa na mcheza dansi katika ulingo wa masumbwi - akiwakumbusha watu huo ulikuwa ni mchezo.
“Aliurejeshea mchezo huo msisimko na kuwa wa maana tena. Alikuwa akiburudisha na alipokuwa kijana alikuwa akizungumza sana. Lakini ilikuwa ni sehemu ya madoido yake.Joe Bugner (Mwanamasumbwi aaliyewahi kupigwa na Ali mara 2)
“Alikuwa ni mwanamichezo zaidi ya mwanamasumbwi. Alikuwa ni mwanamichezo
Frank Bruno
“hatutaweza kumshuhudia bondia mwengine kama alivyokuwa Ali, aliiuweka mchezo wa masumbwi katika ramani”.
“Alifungua njia kwa wanamasumbwi kama mimi kupenda mchezo huo na kujipatia kipato,” alisema Bruno.
George Foreman: Mwanamasumbwi aliyewahi kupambana na Mohammed Ali katika mechi iliyofanyika Zaire (Sasa DRC) kabla ya Ali kuibuka mshindi, anasema kuwa Mohammed Ali alikuwa na ushawishi wa kukufanya umpende. Iwapo usingempenda angekufanyia vituko zaidi ili uweze kumchukia zaidi.
Florah Mosha: Moyo wangu unanung’unika kwa kumpoteza mwanzilishi, bondia hodari, bingwa na shujaa kwa vyovyote vile. Hakuna siku niliingia katka ulingo wa ndondi bila kumkumbuka , alisema katika mtandao wa instagram. Ucheshi, uzuri wako na vinginevyo ndio vitu tutakavyovienzi.Julia Hassan: Kila mara nilihisi Mungu alimfanya Muhammad kuwa mtu muhimu, lakini sijui kwa nini Mungu alinichagua mie kumbeba mwana huyu, wakati alipokuwa mtoto hakuweza kutulia, alitembea na kuzungumza na kufanya kila kitu wakati wake. Akili yake ilikuwa kama upepo unaovuma na kueleka kila sehemu.Rahman Ali: Nduguye Mohammed Ali anasema kuwa marehemu alikuwa akimtaka amrushie mawe, nilidhani ameshikwa na wazimu, lakini mawe hayo angeyakwepa yasimpige kumpiga.John Alex: Ndio mwanamichezo hodari mweusi niliyewahi kumjua na ana umuhimu mkubwa kwa watu wake. Kwa sababu mabilioni ya watu kutoka Afrika, Asia na Arabia wanakupenda lazima ujue majukumu yako.
Jesse Jackson:Walikataa kusikiliza ushuhuda wake kuhusu dini yake. Walijaribu kumnyanyasa, walijaribu kumuathiri kimwili na kiakili.
Bingwa wa zamani wa ngumi za kulipwa uzito wa juu duniani, Mohammad Ali aliyefariki dunia usiku wa kuamkia jana, aliwahi kuzuru nchini Tanzania mwaka 1980.

No comments:

Post a Comment