Monday, October 3, 2016

MAKALA: SANAA YA UCHONGAJI

HAMASA-KAGERA

Leo baada ya kumtembelea moja kati ya wachongaji vinyago na mihuri aliye katika Maspaa ya Bukoba Mjini Bwn.Shafi Mustapha ameweza kutueleza mengi kuhusu shughuli zake za uchongaji na kwa namna anavyoziendesha na changamoto anazo kabiliana nazo.Akiongea na Gazeti la Hamasa Bwn.Shafi Mustapha alielezea kuwa shuguli yake kubwa anayo jishughulisha nayo katika ofisi yake ni uchongaji wa mihuli mbalimbali kama ya Mashuleni,Ofisini au ya mtu binafsi.
  Alizungumzia shughuli hiyo kama shughuli yenye manufaa makubwa kwake na ndoo kitu kinachomfanya aifanye shughuli hiyo kwa kipindi cha muda mrefu mpaka sasa, kwani shughuli hiyo ya uchongaji wa mihuri ndio inayomuwezesha  Bwn.Shafi Mustaph ambaye ni Baba wa watoto sita kuweza kuimudu familiayake katika mahitaji mbalimbali, akizidi kuliambia Gazeti la Hamasa mafanikio aliyo yapata kupitia kazi yake ya uchongaji wa mihuri alisema “kazi hii imenipatia faida kiasi cha kuweza kujenga nyumba yangu mwenyewe”.Akiwa kama moja ya wanafunzi wa kaka yake ambaye pia ni mtaalamu wa kazi hiyo Bwn.Mustapha alisema kutosomea kazi hiyo ya uchongaji wa mihuri ila ni kazi ambayo alifundishwa na kaka yake kipindi cha nyuma na alijiendeleza mpaka sasa ana ofisi yake ambamo huendeshea shughuli zake za uchongaji mihuri kulingana na mahitaji ya wateja wake mbalimbali.
 Akiendelea na mazungumzo Bw.Mustaph alielezea kwa namna kazi hiyo inayoweza kumgharimu hadi mudawa masaa matatu(3)au zaidi kwa jinsi wateja wake wanavyo ipokea na kundi gani ni sehemu kubwa ya wateja wake? Alisema”Soko na wateja wangu wengi ni watu kutoka maofisi mbalimbali,mashuleni na kwa watu binafsi.Ila changamoto kubwa ni kwa namna baadhi ya wateja hao ambavyo bado hawajauthamini ukubwa na ugumu wa kazi hii hivyo hata katika maelewano hupenda kufanyiwa kazi kwa bei ya chini sana kuliko kazi yenyewe”.
 Bwn. Mustapha ambaye ni mkongwe katika sanaa hiyo ya uchongaji wa mihuri alituelezea kwa ufupi kwa namna uchongaji wa muhuri mmoja unavyofanyika, “Shuguli hizi hutegeme na mahitaji ya mteja  lakini kwa muhuri mdogo wa kawaida hatua zake ni kuchonga maneno katika mpira mdogo na maneneo hayo yawe katika mtindo wa kiarabu yaani hutoka kulia kuelekea kushoto na baadaye huja kuwekwa katika kijibao kidogo cha muhuri.Hatua hizi chache huhitaji usanifu na ufundi mkubwa kwa ajili ya kutoa muhuri ambao utamvutia mteja.”



No comments:

Post a Comment