Tuesday, September 20, 2016

Wimbo mpya wa Diamond 'kumfufua' Saida Karoli?


Tangu ulipotoka wimbo wa Salome alioufanya Diamond akitumia vionjo vya wimbo uliofanya vizuri sana ndani na nje ya nchi wa Saida Karoli 'Chambua kama karanga' watu wengi wamekuwa wakihoji kuhusu makubaliano baina ya watu hao wawili yakoje. Haya ndio majibu aliyoyatoa Diamond;-


Diamond amesema kuwa mwanamuziki huyo mkongwe wa nyimbo za asili ana asilimia 25 kwenye pesa ambazo wimbo huo utakuwa unaingiza,

“Kitu tulichokifanya kabla ya kurealise wimbo,tulizungumza na uongozi wake tukawaambia tunafanya ichi,ichi na ichi, kuna kiasi pia tukakitoaili kiende kwake alafu tukampa 25 percent ya publishing kila income ya publishing ikiwa inaingia katika huu wimbo, mama atakuwa anapata percent” Diamond ameiambia Perfect 255.

Saida Karoli alipata mafanikio makubwa kupitia wimbo huo ikiwa ni pamoja na kutumika kwenye filamu ya muandaji maarufu wa Hollywood, Tyler Perry.

No comments:

Post a Comment