Tuesday, September 20, 2016

Historia ya Karagwe kuandikwa upya

Akizungumza na Hamasa mwanzilishi wa siku ya Utamaduni wa Wanyambo ‘alifunguka’  kama ifuatavyo;-

MUANDAAJI - Kazi hii ya kuunda upya historia ya karagwe  lilikuwa wazo la watu wawili ambao ni mimi mwenyewe, Bullet Straton Ruhinda (Sociologist/ Anthropologist) na Edward Frontline Ruhinda (Environmental Engineer). Wazo lilikuwa ni kuandika historia hii kwa kutumia mbinu yaani kutumia mtazamo kwa namna ya kuwapitia wazee na watu wote wenye historia ya Karagwe ili kuweza kuiweka kwenye kumbukumbu kwa kizazi kijacho”. Pia ababu ya wazo hili ilikuwa ni kwamba Karagwe inayo historia kongwe sana hapa Tanzania ukiondoa historia ya ukanda wa Pwani hasa Zanzibar na Kilwa, Karagwe ilifuata kwa ukongwe. Pia Karagwe ni moja kati ya falme  katikaAfrika ya Mashariki hasa  kwa Tanzania..Historia ya Karagwe ukiondoa Prof Katoke na Mzee Pesha, imeandikwa zaidi na wageni wakiaongozwa na Speke, Prof. Birgita Farelius na wengineo. Katika kuikusanya historia hii kulikuwa na mpango wakufanya utamaduni wa Karagwe na Kagera kwa ujumla kuwa chanzo cha utalii. Hii ni pamoja kufufua makumbusho kama Ikulu za Karagwe na kuzifanya kuwa vivutio vya watalii.Vilevile kulikuwepo mpango wa kuzitambua na kuzikusanya mali za kale za karagwe na kuzihifadhi vizuri kwa kizazi kijacho. Baadhi ya mali za kale hizo zipo mikononi mwa watu na nyingine zipo serikalini ila utunzaji wake sio mzuri. Zipo sehemu kama Mtagata, na maeneo ya maziko ya Bakama ambayo yameanza kuharibika yanatakiwa kutunzwa na kuhifadhiwa na bado Kuna mchakato wa kushirikiana na serikali na wadau wengine ambapo tuliona ni vema kuanzisha siku ya utamaduni ambayo itakuwa inaazimishwa kila tarehe 21 Mei ya kila mwaka na huu ni mwaka wa pili mfululizo kuanzia mwaka 2015. Tarehe hiyo kila mwaka kunakuwa na maonyesho ya kitamaduni  na mali za kale toka maeneo mbalimbali ya Karagwe. Kwa kweli mwitikio ni mzuri sana kama  nitakumbuka vizuri mwaka jana watu walisafiri toka Karagwe nzima kuja kuazimisha siku ya tarehe 21 Mei. Mwaka huu imekuwa na ufanisi mkubwa zaidi, watu wamesafiri toka mikoani kuja kushuhudia.. Pia mwaka huu kulikuwa na wawakilishi kutoka nje ya nchi. Ufalme wa Bunyoro  pia falme jirani kama Kianja(Kamachumu), Busubi(Biharamulo) na Bugufi(Ngara). Wote hao wamekuja kwa gharama zao.
Katika harakati zetu tumejaribu kupitia falme za zamani kuangalia jinsi ya kuifanya historia ya Kagera iwe katika nyaraka. Baadhi ya falme tumepitia ni pamoja na Kianja, Kyamutwara na Bugufi.

Aliendelea kwa kusema kuzungumzumzia upande wa uwezeshaji wa Tamasha ambapo alisema, “Kwa asilimia kubwa naliwezesha mimi, wananchi wanachangia kidogo, kwa upande wa Serikali imesaidia sana katika kuweka mazingira ya kufanyika kwa Tamasha”.
Aidha ametoa shukrani kwa Redio za kijamii kama Fadeco na Karagwe kwa mchango wao wa matangazo ya bure kuhusu Tamasha hilo.walipendekeza baadae iwe ya kimkoa. Ndio maana tulifikia hatua ya kwenda katika Falme nyingine kama Bugufi, Kianja na Busubi. Mwakani tamasha linategemea kuhusisha watu wengi zaidi toka mkoani Kagera maana Kagera ni moja na utamaduni unakaribiana sana.


No comments:

Post a Comment