Tuesday, September 20, 2016

Ngeze: Nshomile gani hawasomi Vitabu?

Mzee Pius Ngeze akifanya mahojiano na HamasaTalkshow


NA DIDAS MUGYABUSO

Mzee Pius Ngeze ambaye ni nguli wa siasa nchi, na ameweza kushika nyadhifa kubwa mbalimbali nchini ikiwa pamoja na Ubunge ameongea na HAMASA na kusema baada ya kustaafu siasa aliamua kujikita na kipaji chake cha uandishi, ambapo anamiliki kampuni yake ya uchapishaji wa vitabu iliyopo mjini Bukoba inayoitwa Tanzania Educational Publishers (TEPU). Alisema aliingia kwenye uandishi kwa vile una mchango mkubwa kwani neno lililoandikwa halifutiki milele, na kitabu ni urithi, yeye atakufa lakini vitabu vitabaki ,aliendelea kusema, “watu wengi hawaoni umuhimu wa vitabu, lakini ipo siku wataona umuhimu huo na watavisoma”. Akijibu swali la mwandishi alisema anaandika kukidhi haja, anapoona mahali kuna pengo anapenda alizibe kupitia uandishi huo. Lakini kabla ya kuandika ni lazima afanye utafiti kwenye vyanzo mbalimbali kwani vitabu vyake vingi ni vya kisayansi. Umahiri wake wa kuandika vitabu vya kuelimisha hasa kwenye upande wa kilimo ulimfanya apate tuzo kadhaa kama kutambua mchango wake.
“Ninapenda zaidi kuandika upande wa kilimo kwa kuwa nina digrii ya kitu hicho hivyo anaandika kitu nachokijua, lakini pia si mvivu wa kusoma, naendelea kusoma kila sikuili nipate elimu zaidi”. aliongeza. Soko lake kubwa la vitabu ni Halmashauri za wilaya, na vinasambazwa Tanzania nzima na  nje ya Tanzania. Aidha aliongelea  vitabu alivyowahi kuandika vikapendwa zaidi ambavyo ni ‘Misingi ya kilimo bora’ kilichotoka mwaka 1975 ambacho anasema kinauzika hadi leo, pia kitabu cha ‘Ufugaji wa kuku’, anasema kinauzika sana kila kona Tanzania, na kitabu kingine kinaitwa ‘Silaha 100 za kiongozi’. Aliiambia HAMASA  kuandika kitabu sio lazima uwe na digrii, mtu yeyote anaweza kuandika, kwani Shaban Robert kaandika vitabu vingi vinavyotumika hadi leo pamoja na kwamba hana digrii. Pia vitabu vyake vinalenga zaidiwatu wa vijijini ,  wakulima, wafugaji na wavuvi hivyo teknolojia haijaathiri mauzo ya vitabu, kwani kwa vijijini sio watu wengi wenye smartphone au Tv. Kabla hajamaliza mazungumzo alituachia ‘dongo’ lenye ukweli wana Kagera, “watu wa hapa ‘wahaya’ wanajiita Nshomile, Nshomile gani hawasomi vitabu?” Alihitimisha kwa kusema kuwa  elimu lazima iwepo ya kuhamasisha watu kupenda kusoma tangia wadogo, sio vitabu vya darasani tu kwa ajili ya kushinda mtihani, vitabu vya hadithi mbalimbali pia kwani vinajenga, kwani  usomaji wa vitabu ni chakula cha ubongo, inamuongezea uwezo wa kufikiri na kujenga hoja nyingi na zenye maana Kubwa sana katika maisha ya kawaida ya mwanadamu.

No comments:

Post a Comment