Tuesday, September 20, 2016

MISS KAGERA



Anaitwa Bhoke Maria Tubeti, ni Mrembo anayeshikilia taji la ulimbwende Mkoa wa Kagera, na pia aliweza kuingia 5 bora Miss Lake Zone. HAMASA tulipiga naye stori mbili tatu kutaka kujua maisha yake ya umiss kwa ujumla.Tuliongea naye mambo mengi, kwa ufupi hizi ndizo nukuu muhimu kutoka kwake.
NINI KILIMVUTIA KUSHIRIKI UMISS?
“Tokea niko mtoto napenda mambo ya urembo,ili niweze kutimiza ndoto zangu niliamua kushiriki umiss”
“Napenda kuwa Mwanamitindo wa kimataifa, biashara za urembo, Mungu akijalianitafungua bonge la Saloon Mwanza”
CHANGAMOTO
“Kila kitu unajigharamia mwenyewe na vitu ni expensive, matumiz yanazidi hata zawadi  unayopata”
“Mambo ya kishirikina mkiwa kambini”
ALIA   NA WAANDAAJI
“wandaaji wengi ni waswahili sana, wanataja zawadi na fursa nyingi ila mwisho wa siku hakuna lolote,  kwa mfano mimi  bado sijamaliziwahela yangu ya Miss Lake Zone ila nikapotezea”
“ Kuna haja ya kubadili waandaji na kuwapa watu wengine nafasi ili tupate mabadiliko kwa sababu unakuta muandaji  anaandaa zaidi  ya miaka kumi, lazima atarudia makosa tu”.

No comments:

Post a Comment