Tuesday, September 20, 2016

Kagera Movie kimataifa

NA HAMASA

Baada ya kushuhudia Filamu mbalimbali zilizoigizwa na wasanii mbalimbali kutoka Mjini Bukoba Mkoa wa Kagera sasa waigizaji hao wamejipanga kutoa Filamu itakayoweza kuuzwa kimataifa, tukiongea na mtunzi wa stori ya Filamu hiyo muigizaji nguli kutoka Bukoba na mmiliki wa Tuzo ya Filamu bora Kanda ya Ziwa Victoria, Onyango Ochola ambaye amekwisha tengeneza Filamu mbalimbali Mjini  Bukoba kama Kaburi la Mama na nyingine nyingi, muigizaji huyo mwenye muda mrefu akifanya  sanaa ya Filamu  alizungumzia Filamu hiyo ya Safari Ya Mauti itakua ni moja kati ya kazi kubwa za Filamu alizowahi kufanya maana amejipanga na ni Filamu yenye ubora na viwango vya hali ya juu akilinganisha na zile alizowahi kufanya. Movie hiyo ya Safari Ya Mauti ameizungumzia kama Filamu iliyolenga sana maswala ya kijamii na inayotoa maelekezo katika jamii ili kuenenda katika maadili yanayofaa. Alisema ni Filamu itakayohusisha mazingira mbalimbali nchini Tanzania yakihusisha pia mazingira ya Mkoa wa Kagera pamoja na maeneo mengine nchini Tanzania , Filamu hiyo ni mojakati ya Filamu kubwa za Mji wa Bukoba zilizoshirikisha mastaa mbalimbali wa nchini Tanzania wanao fanya vizuri katika sanaa ya Maigizo, wasanii hao ni kama Hashimu kambi na Dude ,mbali na Filamu hiyo kushirikisha mastaa hao pia imewahusisha waigizaji mbalimbali kutoka Mjini Bukoba ambao pia ni washiriki wa Filamu hiyo, alizungumzia namna alivyo wahusisha wasanii hao kutoka Mjini Bukoba alisema ilimbidi afanye usaili wa kuangalia vipaji vya Kuigiza kwa watu mbalimbali ili kupata washiriki hao katika Filamu hiyo ya Safari Ya Mauti. Usahili huo uliofanyika viwanja vya Linaz Night Club Mjini Bukoba siku ya 25-27/05/2016 ndio uliomuwezesha kupata Wasanii wa kuchezeshwa katika Filamu  hiyo kutoka Mjini Bukoba pia mbali na kupata wasanii hao ilimlazimu awafanyishe mazoezi ili waweze kuiva zaidi katika Filamu hiyo na kufanya vizuri. Aliwaomba wapenzi mbalimbali wa Filamu kuunga mkono juhudi hizo katika Filamu hiyo ili sanaa hiyo  iweze kufika  mbali.

Msanii na mtayarishaji wa Filamu Kagera bwana Onyango Ochola

No comments:

Post a Comment