Tuesday, September 20, 2016

Oddy Paisy akizungumzia muziki wa Bukoba




Odetha Pais 'Oddy Pais' katika pozi


NA HAMASA
Msanii wa nyimbo za Asili na Zuku anayetamba Mjini Bukoba na Vijijini kwa wimbo wake wa asili wa “Taa Rutha” alizungumzia Muziki wa Bukoba na sababu zinazokwamisha  mzikihuo kufika mbali na kutoa wasanii wakubwa zaidi wa kuiwakilisha Bendera ya Tanzania kutoka Bukoba zaidi ya walivyofanya  Saida Karoli, Bk-Sande na wengine wengi. Akizungumza na gazeti la Hamasa msanii huyo wa muziki Odetha Pais maarufu kama Oddy Pais alisema, “Mziki wa Bukoba umepiga hatua kwa kiasi fulani mpaka sasa tofauti na ulivyokua mwanzo enzi za Saida Kaloli,Maua Chenkula na Revina Kasabira kwani kwa sasa wapo wanamuziki wengi Mjini Bukoba wanajihusisha na muziki vilevile wamejituma kutengeneza video zilizo  na ubora zaidi  na miondoko ya muziki wa asili ya Mjini Bukoba  imebadilika sana”.Mwanamuziki huyo Odi Pais anayeandaa matamasha yake mwenyewe na huwashirikisha wasanii mbalimbali wa mbalimbali ndio njia inayomtangaza msanii Mjini Bukobakama  B-Friends na wengine wengi alizungumza kuwa , “Njia ya kuimba katika  majukwaa na
matamasha kwa kiasi kikubwa katika jamii na ndio njia inayomuingizia fedha msanii maana kwa Tanzania hakuna mikakati mingine mizuri ya kumuingizia msanii wa muziki fedha tofauti na kuimba katika matamasha mbalimbali yanayo andaliwa”.
 Aliendelea kusema “Bado mwamko wa wanaKagera ni mgumu, watu hawapendi kukubali vitu vyao na hushobokea  vitu vya nje, hivyo hutupa wakati mgumu wasanii katika kazi zetu au waandaaji wa matamasha kwani ukiandaa tamasha  la wanamuziki wa Bukoba tu inakua ngumu kupata washabiki labda awemo na staa katika tamasha hilo, hivyo washabiki wa mziki waache mazoea na kukariri na wafwatilie vipaji vipya vilivyomo mjini mwao”.
 Akimalizia mahojiano yake na Gazeti la Hamasa msanii huyo aliwaomba mashabiki wa muziki wajiandae kwa kazi zake nzuri zaidi anazo ziandaa.

No comments:

Post a Comment