Tuesday, September 20, 2016

Mdau: Je Kagera inaweza kuondoka katika umaskini wa kipato?

NA JOHNSTONE MWESIGA(MDAU)

Mkoa   wetu   katika   kipindi   cha   kupatikana   uhuru   wa   Tanganyika   baadaye   Tanzania tulikuwa   kwenye   nafasi   nzuri   sana   kiuchumi,   lakini   miaka   ilivyoenda   mbele   mkoa ukashuka na sasa pato la wakaazi wa mkoa wetu limekuwa ni taabu kweli kweli. Na leo mkoa upo kati ya mikoa mitano iliyoko katika hali mbaya ya umaskini. Hii ni kutokana na tafiti mbalimbali na ni za kweli. Sitapenda   kurudia   mengi   ya   wengi   wasemayo   kuhusu   nini   kimetufikisha   hapa   kilammoja  anajua   na kikubwa  ni   kutofanya  kazi  kwa  juhudi,   mkoa   kuwa  ‘locked’   hauna mwingiliano   watu   wengi   kutoka   nje   ya   mkoa   na nje   ya   nchi   ingawa   ndo   mkoa unaoongoza   kwa   kupakana   na   nchi   nyingi.   Hii   ni   kutokana   na   kutokuwa   na  fursa wezeshi ambazo zimekwisha kugunduliwa au kubuniwa na sisi wakazi wa mkoa, ili watu wengi kutoka ndani na nje waje kuwekeza kwazo.

NINI KIFANYIKE ILI MKOA UPANDE KIMAENDELEO?
1. KILIMO Mkoa wa kagera

ni moja ya mikoa yenye uhakika wa mvua na vyanzo vya maji kama mito   na   maziwa   ambayo   ni   support   ya   mimea   ya   mazao   mengi.  Pia   matumizi   ya mbolea hasa samadi na ile ya viwandani, kutokana na uwepo wa fursa hizo na kwa kuwa kuna hali ya hewa nzuri,   ardhi ya kutosha kulima mazao mbalimbali kama matunda, miti, migomba mihogo mbogamboga,mibuni, vanilla na mengne mengi, ila wakazi wa mkoa huu tumekuwa nyuma katika sekta ya kilimo kwa mapana yake.  Ambacho kinaweza kutukwamua katika janga  la umaskini na kuusogeza mbele kiuchumi kwa mkoa wetu. Hivyo tungewekeza kwenye kilimo chenye tija kwa wakulima, mfano zao kuu letu la biashara   kahawa   ambalo   linastawi   karibu   katika   wilaya   zote   za   mkoa   wetu lingefanyiwa mapinduzi halisi kwa kuboresha taasisi zinazosimamia zao hili kuanzia taifa hadi kwenye vyama vya msingi. Tutumie vizuri kituo cha utafiti wa kilimo Maruku, TACRI,   KCU,   KDCU,   ziwe   imara   kwa   ajili   ya   maslahi   ya   wakulima   na   kutoa   elimu inayokidhi katika ukulima wa kisasa. Bei ya kahawa iwe yenye kumpa nafuu ya maisha mkulima.   Haya   si   kwa kahawa   pekee,   iwe   pia   kwa   zao   la   chai   ambalo   kiukweli limepoteza mvuto mkoani kwetu, miwa, vanilla,maua,  miti ya matunda na mbao iwe na kanuni nzuri  za  ulimaji na utunzaji.  Tuige  vyama vingne kama KNCU cha  Kilimanjaro,Mbinga coffee growers, nk.   Mazao   ya   chakula   pia   kilimo   chake   kiboreshwe   tuachane   na   kulima   kimazoea maharage, mahindi, migomba, mihogo, viazi vitamu, mbogamboga hivi vikilimwa kwa ustadi vina soko kubwa. Mfano mhogo unahitajika sana nchi jirani Uganda na Sudan, nadhan huwa  tunaona jinsi  watu wa Buseresere wanavyouza makopa  kule Uganda.Viazi vitamu aina ya karoti ni kirutubisho kizuri kwa afya zetu.   hivyo tufanye tafiti na kutumia matokeo ya tafiti hizo kujikwamua katika kilimo

 2. UTALII  Kagera imejaliwa vivutio vya utalii ambavyo vinaweza kutuingizia pato kama mkoa kupitia makampuni ya kitalii. Vivutio si mpaka vivumbuliwe na wazungu hata sisi tunaweza kugundua maeneo ya vivutio ambavyo ni sehemu ya kuleta watu wenye nia ya kuviona kutoka ndani na nje ya nchi ili tupate pato katika kampuni za kitalii zinazoongoza watalii,pato   la   mkoa   kama   kodi,   na   pato   kwa   wenye   hotel   pamoja   na   wauzaji   wa   vitu mbalimbali watakvyovutiwa navyo wakiwa matembezini. Kama Sikosei Bukoba yapo makampuni yanayotangaza vivutio vya utalii kama  Willy Bukobatours,  Kiroyera  na  Frajo Media, hawa watu  wanajitahidi sana katika kuendeleza utalii Kagera. Ila tuwaunge mkono tuendelee kubainisha maeneo mengine mfano kuna kisiwa kilichopo ziwa Victoria kati ya Kemondo na Bukoba karibu na mwambao wa Maruku.Kinaweza kuwa kivutio kikifanyiwa utafiti kuona kuna aina gani ya wanyama na mimea,   ndege   au   kama   hakuna   ni   wanyama   gan   waletwe   ili   kukidhi   haja   ya   utalii.Maporomoko   ya   mito,   chemi   chemi,   kuendeleza   miambao   ya   maziwa,mapango n.k

3. MICHEZO Michezo ni moja ya sekta muhimu katika kuleta mandeleo ya kiuchumi sehemu husika,michezo inakutanisha watu mbali mbali ,inaboresha mahusiano baina ya watu, michezo inajenga   afya   kwa   wachezaji  pia   inawapatia   wanajamii   kipato  kuptia   kutoa   huduma wakati wa michezo au kushiriki katika michezo husika. Mkoa wetu ni mmoja ya mikoa ambayo iko katika kiwango fulani cha michezo si kizuri au si kibaya sana ila juhudi zinahitajika kuimarisha maana kijumla michezo hatuishabikiisana. Mpira wa miguu tushukuru tuna timu ligi kuu, ila bado tuweze kuwa nazo zaidi ya moja itakuwa vizuri, tumshukuru malinzi na TFF kwa uboreshaji wa uwanja wa kaitaba. Ila   bado   tuhitaji   kuwa   na   viwanja   vingne   vingi   kwa   mkoa   mzima   kwa   michezo mbalimbali, netball, basketball, volleyball, n.k ili tuweze kuvuutia waandaji wa michezo mbali mbali kuandaa michezo yao mkoani kwetu mbali na kwenda kila mwaka Dar es salaam. Tushukuru pia Misenyi kuna kiwanja cha gofu. Kuanzisha matamasha  mbalimbali yenye tija mfano mbio za marathoni mfano Lweu, Marathon,   Kagera   Marathon   au   jina   lingne   lolote   lenye   mvuto.   Hii   ni   kwa   kutafuta wadhamini mfano viwanda vilivyoko  Kagera vikadhamini, Kagera sugar,  Tanica,  Yetuchai, viwanda vya maji na soda na juice vikaweka mkono kudhamini huku vikitangaza bidhaa zake, hata vituo vya redio vilivyoko mkoani takriban vitano vikapewa fursa hiyo....

4. AFYA NA MAZINGIRA
Miji yote ya Kagera haina mpangilio maalumu na usafi wake wa mazingira hauridhishi,hivyo tuwekeze katika kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira uboreshaji wa miundo mbinu ya maji, barabara, stend zetu, upandajimiti, usafi wa kila mara, nyumbani na mtaani, ili ile hali ya hewa nzuri ya Kagera ionekane katika usafi wa mazingira, pia katika afya zikiboreshwa hospitali zetu na kujengwa nyingne kubwa kama ya kansa na ya watu wa orthodox inaweza  kuletamabadiliko makubwa pia katika uchumi wamkoa wetu. Kikubwa ni serikali na wadau kuwapa nafasi wawekezaji na kuhakikisha huduma hizi zinakuwepo.
5.VIWANDA-Tunavyo viwanda vikubwa na vidogo hapa sina mengi maana viwanda vya Kagera sijuimaafisa  masoko  wake wanajua  kufanya  kazi?  Wajitahid  kutafuta masoko ya  nje  nakuboresha brand6.
6.ELIMU- Kila mmoja wetu anaelewa juu ya neno NSHOMILE neno hili lilikuwa na maana sana, kwani jamii yetu ilienda shule awali kuliko wakazi wa mikoa mingine, na kutokana na hilo  tulitegemea   ELIMU  ikawe   nuru   kwa   mkoa   wetu.  Lakini   leo   neno  nshomile limegeuka kama kebehi kwa watu wa Kagera. Ukilisikia tu unatamani kuficha uso, na wameshatujua watu wa nje ya Kagera wanatukejeli kweli kweli. Hebu tujiulize tuna vyuo vya serikali vingapi katika mkoa wetu ukilinganisha na mikoa mingine. Kuna vyuo vya kati ukiachana na vyuo vikuu, mfano chuo cha kodi,chuo cha maendeleo ya jamii, chuo cha Ustawi wa Jamii, Nyuki, Maji, Ardhi, FTC,Uhasibu   na   vingne   vingi,   hivi  sijui   ilikuwa mpango   wa   kuiondoa   Kagera kwenye   ramani   ya   wasomi   maana   utasikia   vyuo   vingi   nilivyovitaja   ni   kigoma, Iringa,Arusha, Kili, Mbeya, Mtwara, Singida, Tabora ndo usiseme, Mwanza Mara, n.k. Ila Kagera ni Kagemu na Katoke. Kwa vyuo vikuu upande wa serikali utasikia wanaplan kuanzisha chuo mara, Katavi Arusha, n.k si KAGERA.Haya yote sawa lakini je sisi tumejipangaje kuwasomesha watoto wetu na sisi ili turudi kama zamani kuondoa aibu hii inayotutafuna?

Maoni ya Mdau:
JOHNSTONE MWESIGA

No comments:

Post a Comment