Tuesday, September 20, 2016

KOMBE LA NG’OMBE KUENDELEA KUTIMUA VUMBI




Pichani: Majengo Warriors (Jezi Nyekundu) Vs Ibosa FC (Jezi ya Bluu)



Ni katika michuano ya Kombe la Ng’ombe lililodhaminiwa na mtu aliyetajwa kwa jina moja ‘Amri’, ambapo michuano inatarajia kwisha mwishoni mwa mwezi wa 9, jumla ya timu zinazoshiriki ni 9, na sasa wapo kwenye hatua za mwisho. Mshindi wa kwanza atapewa dhawadi ya ng’ombe ‘aliyenona’, wa pili ataibukia na kitita cha shilingi laki 2, na wa tatu laki 1. Pichani ni timu za Majengo Warriors na Ibosa FC zikitoana jasho katika uwanja wa shule ya Ibosa, ambapo walitoka sare kwa kufungana bao 1-1, mfungaji wa Ibosa ni Ramadhan Yusuph (Kapirima) na Majengo Warriors ilifungiwa na Fikiri David kupitia faulo ya kiufundi.

No comments:

Post a Comment