Friday, September 23, 2016

POLISI YASAMBARATISHA MKUTANO WA UKAWA KAGERA


Polisi yasema hakuna taarifa za mkutano huo, yawataka kufuata waathiriwa majumbani.
Akizungumza na watu takribani sabini waliokuwa wamesubiri viongozi na wageni taifa kuwasili mjini Bukoba katika viwanja vya shule ya msingi Kashai, afisa upelelezi wa polisi wilaya ya Bukoba, amesema kuwa wameshatoa maelekezo kuwa wafanye mkutano wa ndani, na kama ni kuzungumza na waathiriwa wa tetemeko, wanatakiwa kuwazungukia kwenye maeneo yao.
Awali, Mh. Wilifred Muganyizi Lwakatare, aliwaalika wananchi kuudhuria mkutano huo, wakiwasihi kumuunga mkono kuuliza maswali kwa mwakilishi wa mkuu wa wilaya ambaye angejifika mkutanoni hapo.

No comments:

Post a Comment